Maneno, yaliyoandikwa na kusemwa, na watu watakatifu wa Mungu wakiwa wanaongozwa na Roho Mtakatifu. Maandiko matakatifu yanayotambuliwa rasmi na Kanisa siku hizi ni pamoja na Biblia, Kitabu cha Mormoni, Mafundisho na Maagano, na Lulu ya Thamani Kuu. Yesu na waandishi wa Agano Jipya waliviheshimu vitabu vya Agano Jipya kama maandiko (Mt. 22:29 ; Yn. 5:39 ; 2 Tim. 3:15 ; 2 Pet. 1:20–21 ). Ona pia Wendo katika kiambatisho.
Je, mioyo yetu haikuwaka ndani yetu, wakati alipotufungulia maandiko? Lk. 24:32 .
Mwayachunguza maandiko; kwa sababu mnadhani kwamba ninyi ndani yake mnao uzima wa milele, Yn. 5:39 .
Maneno ya Kristo yatawaeleza mambo yote mpaswayo kuyatenda, 2Â Ne. 32:3 .
Kadiri wengi wanavyoongozwa kuamini maandiko wanakuwa imara na thabiti katika imani, Hel. 15:7–8 .
Wanadamu hukosea katika kuyapinda maandiko na hawayaelewi, M&M 10:63 .
Maneno haya si ya wanadamu wala si ya mwanadamu, bali yangu mimi, M&M 18:34–36 .
Kuibuka kwa kitabu cha Mormoni kunathibitisha kwa ulimwengu kwamba maandiko ni ya kweli, M&M 20:2, 8–12 .
Muda wenu na utumike kwa kujifunza maandiko, M&M 26:1 .
Maandiko yanatolewa kwa ajili ya maelekezo kwa watakatifu, M&M 33:16 .
Maandiko hutolewa kwa wokovu wa wateule, M&M 35:20 .
Fundisheni kanuni za injili yangu, ambazo ziko katika Biblia na Kitabu cha Mormoni, M&M 42:12 .
Sheria zangu juu ya mambo haya zimetolewa katika maandiko yangu, M&M 42:28 .
Lolote wanalosema chini ya mwongozo wa Roho Mtakatifu ni maandiko, M&M 68:4 .
Kuna maandishi mengi matakatifu yaliyotajwa katika maandiko ambayo hatunayo leo, miongoni mwake ni vitabu hivi na waandishi hawa: agano (Ku. 24:7 ), vita vya Bwana (Hes. 21:14 ); Yashari (Yos. 10:13 ; 2 Sam. 1:18 ), matendo ya Sulemani (1 Fal. 11:41 ), Samweli mwonaji (1 Nya. 29:29 ), Nathali nabii (2 Nya. 9:29 ), Shemaya nabii (2 Nya. 12:15 ), Ido nabii (2 Nya. 13:22 ), Yehu (2 Nya. 20:34 ), misemo ya waonaji (2 Nya. 33:19 ), Henoko (Yuda 1:14 ), na maneno ya Zenoki, Neumu, na Zeno (1 Ne. 19:10 ), Zeno (Yak. [KM] 5:1 ), Zenoki na Ezia (Hel. 8:20 ), na kitabu cha ukumbusho (Musa 6:5 ); na nyaraka kwa Wakorintho (1 Kor. 5:9 ), kwa Waefeso (Efe. 3:3 ), na kutoka Laodikia (Kol. 4:16 ), na kutoka Yuda (Yuda 1:3 ).
Yatupasa kuzipata kumbukumbu hizi ili tupate kuyahifadhi maneno yaliyonenwa na manabii, 1 Ne. 3:19–20 .
Yanipasa kuyahifadhi mabamba haya, Yak. (KM) 1:3 .
Vitu hivi vimetunzwa na kuhifadhiwa kwa mkono wa Mungu, Mos. 1:5 .
Vitunze vitu hivi vitakatifu, Alma 37:47 .
Utasoma torati hii mbele ya Israeli wote, Kum. 31:10–13 .
Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, Yos. 1:8 .
Sheria ya Bwana ni kamilifu, huiongoa nafsi, Zab. 19:7 .
Neno lako ni taa ya miguu yangu, Zab. 119:105 .
Maandiko hunishuhudia mimi, Yn. 5:39 .
Maandiko yote hutolewa kwa mwongozo wa Mungu na yafaa kwa mafundisho na maelekezo, 2 Tim. 3:15–16 .
Niliyalinganisha maandiko yote na sisi, ili yapate kuwa kwa manufaa na mafundisho yetu, 1Â Ne. 19:23 .
Moyo wangu hufurahia katika maandiko, 2 Ne. 4:15–16 .
Tunaandika kwa bidii, ili kuwashawishi watoto wetu, na pia ndugu zetu, kuamini katika Kristo, 2Â Ne. 25:23 .
Waliyachunguza maandiko, na hawakusikiliza tena maneno ya huyu mtu mwovu, Yak. (KM) 7:23 (Alma 14:1 ).
Kama siyo kwa ajili ya mabamba haya, lazima tungeliteseka katika ujinga, Mos. 1:2–7 .
Walikuwa wameyachunguza maandiko kwa bidii, ili wapate kujua neno la Mungu, Alma 17:2–3 .
Maandiko yanalindwa ili kuzileta roho katika wokovu, Alma 37:1–19 (2 Ne. 3:15 ).
Neno la Mungu litamwongoza mtu wa Kristo, Hel. 3:29 .
Lolote watakalonena kwa uwezo wa Roho Mtakatifu litakuwa andiko takatifu na uwezo wa Mungu katika wokovu, M&M 68:4 .
Pigeni chapa utimilifu wa injili yangu kwa madhumuni ya kulijenga Kanisa langu na kuwatayarisha watu wangu, M&M 104:58–59 .
Maandiko yaliyotolewa unabii kwamba yatakuja
Vitabu vingine vitakuja, 1Â Ne. 13:39 .
Hamna haja ya kudhani kwamba Biblia ina maneno yangu yote, 2 Ne. 29:10–14 .
Muikubali injili ya Kristo, itakayowekwa mbele yenu katika kumbukumbu zile zitakazokuja, Morm. 7:8–9 .
Heri yule ambaye atadhihirisha jambo hili, Morm. 8:16 .
Yaandike mambo haya nami nitayaonyesha katika wakati wangu mwenyewe utakapofika, Eth. 3:27 (Eth. 4:7 ).