Misaada ya Kujifunza
Ezekieli


Ezekieli

Nabii aliyeandika kitabu cha Ezekieli katika Agano la Kale. Yeye alikuwa kuhani katika familia ya Sadoki na ni mmoja wa mateka wa Kiyahudi waliohamishwa na Nebukadneza. Aliishi pamoja na wakimbizi wa Kiyahudi katika Babilonia na alitoa unabii katika kipindi cha miaka ishirini na miwili, tangu mwaka 592 hadi mwaka 570 K.K.

Kitabu cha Ezekieli

Kitabu cha Ezekieli chaweza kugawanywa katika mafungu manne. Mlango wa 1–3 inaelezea juu ya Ono la Mungu na wito wa Ezekieli wa kuhudumu; mlango wa 4–24 inanena juu ya hukumu za Yerusalemu na sababu ya kutolewa kwake; mlango wa 25–32 inatangaza hukumu juu ya mataifa; na mlango wa 33–48 imeandikwa maono ya Israeli ya siku za mwisho.