Misaada ya Kujifunza
Waamuzi, Kitabu Cha


Waamuzi, Kitabu Cha

Kitabu katika Agano la Kale. Kitabu cha Waamuzi kinajishughulisha na Waisraeli kutoka kifo cha Yoshua hadi kuzaliwa kwa Samweli.

Mlango wa 1–3 ni utangulizi wa kitabu chote cha Waamuzi. Inaelezea kwamba kwa sababu Waisraeli hawakuwafukuza maadui zao (Amu. 1:16–35), Waisraeli lazima wapatwe na matokeo yake; kukosa imani, kufunga ndoa na wasioamini, na ibada za sanamu. Mlango wa 4–5 inahusu matukio ya Debora na Baraka, walioikomboa Israeli kutoka kwa Wakanaani. Mlango wa 6–8 ni matukio ya Gideoni yenye kukuza imani, ambaye Mungu alimbariki ili aikomboe Israeli kutoka kwa Wamidiani. Katika mlango wa 9–12, watu kadhaa tofauti wanatumika kama waamuzi katika Israeli, katika wakati ambao Waisraeli wengi walikuwa katika ukengeufu na wkitawaliwa na watawala wageni. Mlango wa 13–16 inasimulia juu ya kuinuka na kuanguka kwa mwamuzi wa mwisho, Samsoni. Milango ya mwisho, 17–21, inaweza kuelezewa kama ni kiambatisho ambacho kinafichua kina cha dhambi za Israeli.