Kumpenda, kumnyenyekea, kumtumikia, na kujitoa kwa Mungu (M&M 20:19 ). Kuabudu kunajumuisha sala, kufunga, ibada ya kanisani, kushiriki katika ibada za injili, na matendo mengine yanayoonyesha kuabudu na upendo kwa Mungu.
Watamwabudu Baba katika roho na katika kweli, Yn. 4:23 .
Mwabuduni yeye aliyezifanya mbingu na dunia, Ufu. 14:7 (M&M 133:38–39 ).
Mwabuduni yeye kwa uwezo, akili, na nguvu zenu zote, 2Â Ne. 25:29 .
Waliamini katika Kristo na walimwabudu Baba katika jina lake, Yak. (KM) 4:5 .
Zeno alifundisha kwamba watu wanapaswa kusali na kuabudu katika mahali pote, Alma 33:3–11 .
Mwabudu Bwana, katika mahali popote utakapokuwa, katika roho na katika kweli, Alma 34:38 .
Watu walianguka miguuni pa Yesu na wakamwabudu, 3Â Ne. 11:17 .
Watu wote lazima watubu, wamwamini Yesu Kristo, na kumuabudu Baba katika jina lake, M&M 20:29 .
Ninawapa maneno haya ili mpate kufahamu na kujua namna ya kuabudu, na kujua nini mnachokiabudu, M&M 93:19 .