Mamlaka na uwezo ambao Mungu humpa mwanadamu ili atende katika mambo yote kwa ajili ya wokovu wa mwanadamu (M&M 50:26–27 ). Waumini wa Kanisa wanaume walio na ukuhani wametengwa katika akidi nao wamepewa mamlaka ya kufanya ibada na shughuli fulani za kiutawala katika Kanisa.
Mimi nimewachagua ninyi, Yn. 15:16 .
Mmejengwa muwe nyumba ya kiroho, ukuhani mtakatifu, 1Â Pet. 2:5 .
Ninyi ni zao teule, ukuhani wa kifalme, 1Â Pet. 2:9 (Ku. 19:6 ).
Wanaume huitwa kama makuhani wakuu kwa sababu ya imani na matendo yao mema yanayopita kiasi, Alma 13:1–12 .
Ninawapa ninyi uwezo wa kubatiza, 3Â Ne. 11:21 .
Ninyi mtakuwa na uwezo wa kutoa Roho Mtakatifu, Moro. 2:2 .
Nitaufunua kwenu ukuhani, kwa mkono wa Eliya, M&M 2:1 (JS—H 1:38 ).
Bwana alithibitisha ukuhani juu ya Haruni na kizazi chake, M&M 84:18 .
Ukuhani huu mkuu zaidi huhudumia injili, M&M 84:19 .
Alimchukua Musa kutoka katikati yao, na Ukuhani Mtakatifu pia, M&M 84:25 .
Kiapo na agano la ukuhani vinaelezwa, M&M 84:33–42 .
Ukuhani umedumu kupitia safu ya uzao wa baba zenu, M&M 86:8 .
Katika Kanisa kuna kuhani mbili, M&M 107:1 .
Ukuhani wa kwanza ni Ukuhani Mtakatifu, kwa Mfano wa Mwana wa Mungu, M&M 107:2–4 .
Haki za ukuhani zimeungana na hazitenganishwi na nguvu za mbinguni, M&M 121:36 .
Hakuna nguvu au uwezo unaoweza au upaswao kudumishwa kwa njia ya ukuhani isipokuwa tu kwa ushawishi na upendo usio unafiki, M&M 121:41 .
Kila mwanaume muumini wa kanisa mwenye kustahili anaweza kupokea ukuhani, TR 2 .