Misaada ya Kujifunza
Kiri, Kukiri


Kiri, Kukiri

Maandiko hutumia neno kukiri katika njia zipatazo mbili. Katika maana moja, kukiri ni mtu kueleza imani yake katika kitu fulani, kama vile kukiri kwamba Yesu ndiye Kristo (Mt. 10:32; Rum. 10:9; 1 Yoh. 4:1–3; M&M 88:104).

Katika maana nyingine, kukiri ni mtu kukubali hatia, kama vile katika maungamo ya dhambi. Ni wajibu wa watu wote kuungama dhambi zao kwa Bwana na kupata msamaha Wake (M&M 58:42–43). Inapokuwa muhimu, dhambi yapaswa zikiriwa kwa mtu au watu uliowakosea. Dhambi kubwa yapaswa zikiriwe kwa viongozi wa Kanisa (hasa askofu).