Misaada ya Kujifunza
Batiza, Ubatizo


Batiza, Ubatizo

Neno lililotumika katika maandishi halisi ya Kiyunani linaanisha “chovya” au “zamisha.” Ubatizo kwa uzamisho katika maji na mtu mwenye mamlaka ni ibada ya kwanza ya injili na ni ya muhimu ili kuwa muumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Hutanguliwa na imani katika Yesu Kristo na katika toba. Ni lazima ufuatiwe na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu ili uweze kuwa kamili (2 Ne. 31:13–14). Ubatizo kwa maji na Roho ni muhimu kabla mtu hajaingia katika ufalme wa selestia. Adamu alikuwa mtu wa kwanza kubatizwa (Musa 6:64–65). Yesu pia alibatizwa ili kutimiza haki yote na ili kuonyesha njia kwa ajili ya wanadamu wote (Mt. 3:13–17; 2 Ne. 31:5–12).

Kwa sababu si watu wote duniani hupata nafasi ya kuipokea injili wakiwa duniani, Bwana ametoa mamlaka ubatizo kufanyika kwa watu walio hai kwa niaba ya wale waliokufa. Kwa hiyo, wale waipokeao injili katika ulimwengu wa roho wanaweza kustahili kuingia katika ufalme wa Mungu.

Muhimu

Ubatizo kwa kuzamishwa

Ubatizo kwa ajili ya maondoleo ya dhambi

Mamlaka sahihi

Sifa zinazotakiwa kwa ajili ya ubatizo

Agano lifanywalo kwa njia ya ubatizo

Ubatizo kwa ajili ya wafu

Ubatizo siyo kwa ajili ya watoto wachanga