Misaada ya Kujifunza
Hekalu la Kirtland, Ohio (Marekani)


Hekalu la Kirtland, Ohio (Marekani)

Hekalu la kwanza lililojengwa na kanisa katika nyakati za sasa. Watakatifu walilijenga huko Kirtland, kulingana na amri ya Bwana (M&M 94:3–9). Dhumuni mojawapo lilikuwa ni kupata mahali ambapo waumini wa Kanisa wanaostahili waweze kupokea nguvu za kiroho, mamlaka, na maarifa (M&M 109–110). Liliwekwa wakfu, mnamo 27 Machi 1836; sala ya kuweka wakfu ilitolewa na Joseph Smith Nabii kwa ufunuo (M&M 109). Bwana alitoa mafunuo kadhaa yaliyo muhimu na kurejesha funguo za ukuhani zilizohitajika katika hekalu hili (M&M 110; 137). Halikutumiwa kwa ibada kamilifu za hekalu kama zinavyotolewa katika mahekalu siku hizi.