Ruhusa iliyotolewa kwa wanaume duniani walioitwa au kutawazwa ili kutenda kwa ajili ya, na kwa niaba ya Mungu Baba au Yesu Kristo katika kutenda kazi ya Mungu.
Mimi nimekutuma, Ku. 3:12–15 .
Utanena hayo yote nikuagizayo, Ku. 7:2 .
Akawapa wanafunzi kumi na wawili uwezo, Mt. 10:1 .
Si ninyi mlionichagua mimi, bali mimi nimewachagua ninyi, na kuwatawaza, Yn. 15:16 .
Nefi na Lehi walihubiri kwa mamlaka makubwa, Hel. 5:18 .
Nefi, mwana wa Helamani, alikuwa mtu wa Mungu, mwenye uwezo mkubwa na mamlaka kutoka kwa Mungu, Hel. 11:18 (3Â Ne. 7:17 ).
Yesu alitoa uwezo na mamlaka kwa Wanefi kumi na wawili, 3 Ne. 12:1–2 .
Joseph Smith aliitwa na kutawazwa na Mungu, M&M 20:2 .
Hakuna atakaye hubiri injili yangu au kulijenga Kanisa langu isipokuwa ametawazwa nayo ijulikane kwa kanisa ya kuwa anayo mamlaka, M&M 42:11 .
Wazee wahubiri injili, wakitenda katika mamlaka, M&M 68:8 .
Ukuhani wa Melkizedeki unayo mamlaka ya kuhudumu katika mambo ya kiroho, M&M 107:8, 18–19 .
Lile lifanywalo kwa mamlaka ya kiungu huwa sheria, M&M 128:9 .