Misaada ya Kujifunza
Ibilisi


Ibilisi

Shetani. Ibilisi ndiye adui wa haki na wa wale watafutao kutenda mapenzi ya Mungu. Huyu ni mwana halisi wa kiroho wa Mungu na wakati fulani alikuwa malaika mwenye mamlaka mbele za Mungu (Isa. 14:12; 2 Ne. 2:17). Hata hivyo, yeye aliasi kule mbinguni kabla ya maisha ya hapa duniani na akashawishi theluthi moja ya watoto wa kiroho wa Baba ili waasi pamoja naye (M&M 29:36; Musa 4:1–4; Ibr. 3:27–28). Wakafukuzwa kutoka mbinguni, wakanyimwa nafasi ya kupata miili yenye kufa na kupata uzoefu wa maisha ya mwili wenye kufa, nao watalaaniwa milele. Toka wakati ibilisi alipofukuzwa kutoka mbinguni, yeye wakati wote amekuwa akitafuta kuwadanganya wanaume na wanawake wote na kuwapeleka mbali na kazi za Mungu ili apate kuwafanya wanadamu wote wawe na huzuni kama yeye alivyo (Ufu. 12:9; 2 Ne. 2:27; 9:8–9).

Kanisa la ibilisi

Kila ovu na shirikisho la kilimwengu duniani ambalo hupotosha injili safi na kamili na ambalo hupingana na Mwanakondoo wa Mungu.