Misaada ya Kujifunza
Ufalme wa Mungu au Ufalme wa Mbinguni


Ufalme wa Mungu au Ufalme wa Mbinguni

Ufalme wa Mungu duniani ni Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho (M&M 65). Madhumuni ya Kanisa ni kuwaandaa wanachama wake kuishi milele katika ufalme wa selestia au ufalme wa mbinguni. Hata hivyo, maandiko wakati mwingine huliita Kanisa ufalme wa mbinguni, yakimaanisha kwamba Kanisa ni ufalme wa mbinguni juu ya dunia.

Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho ndiyo ufalme wa Mungu duniani, lakini kwa sasa ni ufalme wa kidini pekee. Wakati wa Milenia, ufalme wa Mungu utakuwa wa kisiasa na wa kidini.