Misaada ya Kujifunza
Wafilipi, Waraka kwa


Wafilipi, Waraka kwa

Barua ambayo Paulo aliwaandikia Watakatifu wa Filipi wakati alipokuwa gerezani Roma kwa mara ya kwanza. Sasa ni kitabu cha Wafilipi katika Agano Jipya.

Mlango wa 1 una salamu za Paulo na mafundisho yake juu ya umoja, unyenyekevu, na uvumilivu. Mlango wa 2 unasisitiza kwamba wote watainama kwa Kristo na kila mtu lazima autafute wokovu wake mwenyewe. Katika Mlango wa 3, Paulo anasema kwamba yeye amejitolea dhabihu mambo yote kwa ajili ya Kristo. Katika Mlango wa 4, Paulo anawashukuru Watakatifu wa Filipi kwa msaada wao.