Misaada ya Kujifunza
Amri Kumi


Amri Kumi

Sheria kumi zilizotolewa na Mungu kupitia nabii Musa ili kudhibiti tabia za kimwili.

Jina la Kiebrania kwa amri hizi ni “Maneno Kumi.” Pia zinaitwa Agano (Kum. 9:9) au ushuhuda (Ku. 25:21; 32:15). Namna Mungu alivyotoa Amri Kumi kwa Musa, na kupitia yeye kwenda kwao Waisraeli, inaelezwa katika Ku. 19:9–20:23; 32:15–19; 34:1. Amri hizi zilikuwa zimechongwa juu ya mabamba mbili ya mawe, ambazo ziliwekwa katika Sanduku; kwa sababu hiyo Sanduku hilo liliitwa Sanduku la Agano (Hes. 10:33). Bwana, akinukuu kutoka Kum. 6:4–5 na Law. 19:18 amezifupisha Amri Kumi hizi katika “amri kuu mbili” (Mt. 22:37–39).

Amri kumi hizi zimerudiwa tena katika ufunuo wa siku za mwisho (TJS, Ku. 34:1–2, 14 [Kiambatisho]; Mos. 12:32–37; 13:12–24; M&M 42:18–28; 59:5–13).