Misaada ya Kujifunza
Pasaka


Pasaka

Sikukuu ya Pasaka iliwekwa ili kuwasaidia wana wa Israeli kukumbuka wakati malaika mwangamizaji alipopita juu ya nyumba zao na kuwakomboa kutoka kwa Wamisri (Ku. 12:21–28; 13:14–15). Wanakondoo wasio na doa, ambao damu yao ilitumika kama ishara ya kuwaokoa Israeli hapo kale, ni ishara ya Yesu Kristo, Mwanakondoo wa Mungu, ambaye dhabihu yake imewakomboa wanadamu wote.