Hasira ni onyesho la tabia ya ukali. Bwana aliwatahadharisha watakatifu Wake kudhibiti hasira zao (Mt. 5:22 ). Si mzazi wala mtoto anayepaswa kuwatukana wengine katika familia. Katika maandiko, hasira daima imepewa sura ya moto (2Â Ne. 15:25 ; M&M 1:13 ).
Na Kaini akaghadhibika sana, na uso wake ukakunjamana, Mwa. 4:5 .
Bwana si mwepesi wa hasira, na ni mwingi wa rehema, Zab. 145:8 .
Jawabu la upole hugeuza hasira, Mit. 15:1 .
Mtu wa hasira huchochea ugomvi, bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi, Mit. 15:18 (Mit. 14:29 ).
Kwa ajili ya jina langu nitaahirisha hasira yangu, Isa. 48:9 .
Nimewanyooshea mikono yangu watu wanikasirishao daima, Isa. 65:2–3 .
Yeyote akupigaye shavu lako la kuume, mgeuzie na jingine pia, Mt. 5:39 .
Nanyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu wakakasirika, Efe. 6:4 .
Kwa sababu nimewaambia ukweli, mnanikasirikia, Mos. 13:4 .
Nitawatembelea watu hawa katika hasira yangu, Alma 8:29 .
Hasira yake haiwaki dhidi ya yeyote isipokuwa wale wasiokiri mkono wake katika mambo yote, M&M 59:21 .
Mimi, Bwana, nimewakasirikia waovu, M&M 63:32 .