Misaada ya Kujifunza
Talaka


Talaka

Kikomo cha ndoa kwa njia ya mamlaka ya kiserikali au sheria ya kidini. Kulingana na Agano Jipya, Mungu aliruhusu talaka chini ya masharti fulani kwa sababu ya ugumu wa mioyo ya watu; hata hivyo, kama Yesu alivyoelezea, “tangu mwanzo haikuwa hivyo” (Mt. 19:3–12). Maandiko kwa ujumla yanatushauri dhidi ya talaka na yanawashauri waume na wake kupendana kwa haki (1 Kor. 7:10–12; M&M 42:22).