Nefi, Mwana wa Helamani Ona pia Helamani, Mwana wa Helamani; Lehi, Mmisionari wa Kinefi Katika Kitabu cha Mormoni, ni nabii Mnefi na mmsionari. Alikuwa ni mwana mkubwa wa Helamani, Hel. 3:21. Aliteuliwa kuwa mwamuzi mkuu, Hel. 3:37. Yeye na kaka wa Lehi waliwaongoa Walamani wengi katika injili, Hel. 5:18–19. Alizingirwa kwa moto na kufunguliwa gerezani, Hel. 5:20–52. Alisali juu ya mnara wake wa bustani, Hel. 7:6–10. Alifichua mauaji ya mwamuzi mkuu, Hel. 8:25–28; 9:1–38. Alipewa uwezo mkubwa na Bwana, Hel. 10:3–11. Aliomba njaa kwa Bwana na kukoma kwa njaa hiyo, Hel. 11:3–18.