Muziki
Wazee wa Israeli (Wanaume)


170

Wazee wa Israeli

Wanaume

Kwa ujasiri

1. Wazee wa Israeli twendeni

Popote tuwasake wenye haki,

Penye jangwa, bahari na misitu,

Tuwalete Sayuni wawe huru.

[Chorus]

O! Babiloni, Babiloni twakuaga;

Milima ya Efraemu twaenda.

2. Mavuno mengi wavunaji haba;

Tukiungana yote twayaweza.

Tutenganishe nganona magugu

Toka kifungoni wawekwe huru.

[Chorus]

O! Babiloni, Babiloni twakuaga;

Milima ya Efraemu twaenda.

3. Tuwatembelee nao maskini

Wenye njaa na wale wenye dhiki;

Tuwafariji kwa injili yake

Tuwaonyeshe njia ya milele.

[Chorus]

O! Babiloni, Babiloni twakuaga;

Milima ya Efraemu twaenda.

Maandishi: Cyrus H. Wheelock, 1813–1894

Muziki: Thomas H. Bayly, 1797–1839, umefanyiwa marekebisho

Mafundisho na Maagano 133:7–9, 14

Mafundisho na Maagano 75:2–5