170
Wazee wa Israeli
Wanaume
Kwa ujasiri
1. Wazee wa Israeli twendeni
Popote tuwasake wenye haki,
Penye jangwa, bahari na misitu,
Tuwalete Sayuni wawe huru.
[Chorus]
O! Babiloni, Babiloni twakuaga;
Milima ya Efraemu twaenda.
2. Mavuno mengi wavunaji haba;
Tukiungana yote twayaweza.
Tutenganishe nganona magugu
Toka kifungoni wawekwe huru.
[Chorus]
O! Babiloni, Babiloni twakuaga;
Milima ya Efraemu twaenda.
3. Tuwatembelee nao maskini
Wenye njaa na wale wenye dhiki;
Tuwafariji kwa injili yake
Tuwaonyeshe njia ya milele.
[Chorus]
O! Babiloni, Babiloni twakuaga;
Milima ya Efraemu twaenda.
Maandishi: Cyrus H. Wheelock, 1813–1894
Muziki: Thomas H. Bayly, 1797–1839, umefanyiwa marekebisho