Muziki
Lo! Mlimani Kumora


9

Lo! Mlimani Kumora

Kwa kutafakari / Kwa ari

1. Malaika wa juu

Kavunja kimya chake;

Kashuka kwenye mbingu,

Haya maneno yake:

Lo! Mlimani Kumora

Maandiko yamefichwa.

Lo! Mlimani Kumora

Maandiko yamefichwa.

2. Na kwa muda mrefu

Alificha Moroni;

Akingojea Mungu

Aitolee amri.

Itafunuliwa tena

Kufanya njia ya Bwana.

Itafuunuliwa tena

Kufanya njia ya Bwana.

3. Inazungumzia

Uzao wa Yusufu

Na yale mataifa,

Yaliyo mapotevu.

Na utimilifu huo,

Wa injili yake Kristo.

Na utimilifu huo

Wa injili yake Kristo.

4. Sasa ndiyo wakati,

Uliotarajiwa;

Ulimwengu utii,

Giza litatoweka.

Kitabu kifunguliwe,

Duniani kiangaze.

Kitabu kifunguliwe,

Duniani kiangaze.

5. Tazama Israeli

Watakusanywa kwao

Watajenga kwa mali

Yerusalemu yao,

Na Sayuni itang’aa,

Ukweli ikieneza.

Na Sayuni itanga’a,

Ukweli ikieneza.

Maandishi: Parley P. Pratt, 1807–1857

Muziki: John E. Tullidge, 1806–1873

Joseph Smith—Historia ya 1:30–34

Mafundisho na Maagano 128:20