Muziki
Mungu Kamtuma Kwetu


103

Mungu Kamtuma Kwetu

Kwa heshima

1. Mungu kamtuma kwetu—

Mpatanishaji Yesu—

Kutuelekeza njia

Ya kurudi kwake Baba.

2. Na akawa mwanadamu,

Akakubali adhabu.

Akafa bila hatia,

Kuifidia sheria.

3. Upendo mtakatifu!

Nastahili kushukuru,

Kwamba kwa thabihu yake

Nakaa moyoni mwake.

4. Kwa mwenendo anataka

Nijiweke kama mwana,

Ninyenyekee nifunzwe

Na Mtakatifu pekee.

5. Sakramenti twashiriki

Dhabihu twatafakari,

Kwamba neno twatimiza

Na kumkumbuka Bwana.

Maandishi: Edward P. Kimball, 1882–1937

Muziki: Alexander Schreiner, 1901–1987. © 1948 IRI

Yohana 3:16–17

Mafundisho na Maagano 34:3