Muziki
Kaa Nami!


87

Kaa Nami!

Kwa unyenyekevu

1. Kaa nami! Kwani kumekuchwa;

Usiniache gizani, Bwana!

Wanaposhindwa wasaidizi,

Auni wa kweli, kaa nami!

2. Siku zinayoyoma haraka.

Duniani raha hufifia.

Naona mabadiliko mengi;

Ewe Mwaminifu, kaa nami!

3. Kila saa ninakuhitaji.

Nani atamshinda Shetani?

Mwimo wangu, mwingine hakuna,

Kila hali kaa nami, Bwana!

Maandishi: Henry F. Lyte, 1793–1847

Muziki: William H. Monk, 1823–1889

Luka 24:29

Yohana 15:4–12