Muziki
Mahekalu ya Sayuni


162

Mahekalu ya Sayuni

Kwa ujasiri

1. Mahekalu ya Sayuni

Yang’ara utukufu,

Njia ya kwenda mbinguni,

Alama ya uungu.

Taswira ya kuvutia

Yatuita kuomba;

Watiifu wa ahadi,

Pale tutatumika.

2. Mungu Baba wa rehema,

Tutakase twaomba;

Bariki dhamira yetu

Ya ndugu kuokoa,

Hadi siku watiifu,

Wote tuliofungwa

Kwa pingu za selestia,

Tuziimbe hosana.

3. Mbingu, imba kwa sauti,

Nyimbo za kumsifu

Mfalme Imanueli!

Imba Watakatifu!

Milima ishangilie

Na konde zifurahi,

Nyota nazo zimsifu

Ameshinda kaburi.

Maandishi: Archibald F. Bennett, 1896–1965. © 1948 IRI

Muziki: Alexander Schreiner, 1901–1987. © 1948 IRI

Mafundisho na Maagano 138:47–48

Mafundisho na Maagano 128:22–24