Muziki
Nastaajabu


106

Nastaajabu

Kwa kutafakari

1. Nastaajabu upendo wa Yesu kwangu,

Nashangaa neema yake timilifu.

Yasisimua kwamba alisulubiwa,

Kwa ajili yangu, aliteswa na kufa.

[Chorus]

Ni ajabu kwangu angenithamini

Kiasi cha kufa!

Ni ajabu kwangu, ajabu sana!

2. Nastaajabu kwamba angetoka juu

Kuokoa nafsi kiburi kama yangu,

Kwamba upendo wake angenionesha,

Kunikomboa, hata kunihalalisha.

[Chorus]

Ni ajabu kwangu angenithamini

Kiasi cha kufa!

Ni ajabu kwangu, ajabu sana!

3. Nawaza mikono yake ilivyochomwa!

Nisahauje upendowe na huruma?

Hata! Nitamtukuza na kumsifu,

Hadi miguuni nitapomsujudu.

[Chorus]

Ni ajabu kwangu angenithamini

Kiasi cha kufa!

Ni ajabu kwangu, ajabu sana!

Maandishi na muziki: Charles H. Gabriel, 1856–1932

Mosia 3:5–8

Yohana 15:13