Muziki
Israeli, Mnaitwa


7

Israeli, Mnaitwa

Kwa ari

1. Israeli, mnaitwa

Na Mwenyezi mtubu.

Babiloni yaanguka;

Inakuja hukumu.

Njooni humu Sayuni,

Kabla yake gadhabu.

Njooni humu Sayuni,

Kabla yake gadhabu.

2. Israeli, sikiliza

Bwana asema nawe!

Asubuhi yaangaza

Kwa Wateule wote.

Njooni humu Sayuni,

Ndani mfurahie.

Njooni humu Sayuni,

Ndani mfurahie.

3. Israeli, malaika

Toka juu washuka,

Wakiwapa Wema nguvu

Ya kurudi kwa Baba.

Njooni humu Sayuni,

Bwana wenu yu aja.

Njooni humu Sayuni,

Bwana wenu yu aja.

4. Israeli, msibaki

Katika dhambi zenu!

Ona! Hukumu ya haki

Yaja hivi karibu.

Njooni humu Sayuni!

Bwana Mungu msifu.

Njooni humu Sayuni!

Bwana Mungu msifu.

Maandishi: Richard Smyth, 1838–1914

Muziki: Charles C. Converse, 1832–1918

Mafundisho na Maagano 133:7–16