Muziki
Nyimbo za Moyoni


160

Nyimbo za Moyoni

Kwa furaha

1. Nyimbo za moyoni

Sote tutaimba

Kwa pamoja nyumbani kwetu,

Huko tutaishi

Bila kutengana,

Daima na wapendwa wetu!

Huko tutaishi,

Nyimbo za moyoni

Tutaimba nyumbani kwetu.

2. Furaha ni yetu

Haielezeki,

Tutaimba mara kwa mara.

Tukiwapa busu,

Na kuwafariji

Ndugu waliotangulia.

Tukiwapa busu,

Furaha ni yetu,

Ndugu waliotangulia.

3. Tutaona mengi,

Huko selestia,

Na hayaelezeki kamwe.

Roho zitakiri

Wingi wa furaha

Katika nyimbo zenye shangwe.

Roho zitakiri,

Tutaona mengi

Katika nyimbo zenye shangwe.

4. Nyimbo gani bora

Na ukaribisho

Twapata pendo likijiri!

Tukiwa na raha

Na tuwapendao

Kwa wazazi wetu mbinguni!

Tukiwa na raha,

Nyimbo gani bora,

Kwa wazazi wetu mbinguni!

Maandishi: Joseph L. Townsend, 1849–1942

Muziki: William Clayson, 1840–1887

Mafundisho na Maagano 76:58–66, 70

1 Wakorintho 2:9