Muziki
Hesabu Baraka


137

Hesabu Baraka

Kwa uchangamfu

1. Wimbi la maisha likutosapo,

Unakata tamaa ushindwapo,

Hesabu baraka, kwa mojamoja,

Wema wa Mungu utakushangaza.

[Chorus]

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Zihesabu;

Ona ya Bwana.

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Hesabu baraka;

Ona ya Bwana.

2. Je, unaelemewa na mzigo?

Msalaba wakushinda uzito?

Hesabu baraka; shaka ziishe,

Na kisha utaimba siku zote.

[Chorus]

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Zihesabu;

Ona ya Bwana.

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Hesabu baraka;

Ona ya Bwana.

3. Uwaonapo wengine na mali,

Kumbuka ahadi zake Mwokozi.

Hesabu baraka; wingi wa pesa

Haununui ufalme wa Bwana.

[Chorus]

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Zihesabu;

Ona ya Bwana.

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Hesabu baraka;

Ona ya Bwana.

4. Hivyo matatizo yakukumbapo,

Mungu yupo nawe, usife moyo.

Hesabu baraka; na utajaliwa

Malaika watakusaidia.

[Chorus]

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Zihesabu;

Ona ya Bwana.

Zihesabu;

Kwa mojamoja.

Hesabu baraka;

Ona ya Bwana.

Maandishi: Johnson Oatman, Jr., 1856–1922

Muziki: Edwin O. Excell, 1851–1921

Mafundisho na Maagano 78:17–19

Alma 34:38