Muziki
Kwa Milima Twakutukuza


8

Kwa Milima Twakutukuza

Kwa shauku

1. Kwa milima twakutukuza

Ewe, Mungu wetu;

Unatuwezesha sana

Katika kazi zetu.

Waileta Israeli

Kwenye nchi yao.

[Chorus]

Kwa milima twakutukuza,

Ewe, Mungu wetu.

2. Mikononi mwa waonevu

Tumenyanyasika;

Umekuwa msaada

Wa kutuimarisha,

Tukapita maadui

Katikati yao.

[Chorus]

Kwa milima twakutukuza,

Ewe, Mungu wetu.

3. Umetuongoza salama

Hadi kwenye kinga

Ukiwa mlinzi wetu

Tangu tulikotoka.

Kwa ajili ya miamba,

Mabonde, na mito,

[Chorus]

Kwa milima twakutukuza,

Ewe, Mungu wetu.

4. Sisi twauchunga mnara

Nuru isizime;

Sisi ni waangalizi

Chini ya anga kete.

Miamba yajasirisha,

Kwa ya kwako fimbo;

[Chorus]

Kwa milima twakutukuza,

Ewe, Mungu wetu.

Maandishi: Felicia D. Hemans, 1793–1835; yamefanyiwa marekebisho na Edward L. Sloan, 1830–1874

Muziki: Evan Stephens, 1854–1930

Zaburi 95:1–7