8
Kwa Milima Twakutukuza
Kwa shauku
1. Kwa milima twakutukuza
Ewe, Mungu wetu;
Unatuwezesha sana
Katika kazi zetu.
Waileta Israeli
Kwenye nchi yao.
[Chorus]
Kwa milima twakutukuza,
Ewe, Mungu wetu.
2. Mikononi mwa waonevu
Tumenyanyasika;
Umekuwa msaada
Wa kutuimarisha,
Tukapita maadui
Katikati yao.
[Chorus]
Kwa milima twakutukuza,
Ewe, Mungu wetu.
3. Umetuongoza salama
Hadi kwenye kinga
Ukiwa mlinzi wetu
Tangu tulikotoka.
Kwa ajili ya miamba,
Mabonde, na mito,
[Chorus]
Kwa milima twakutukuza,
Ewe, Mungu wetu.
4. Sisi twauchunga mnara
Nuru isizime;
Sisi ni waangalizi
Chini ya anga kete.
Miamba yajasirisha,
Kwa ya kwako fimbo;
[Chorus]
Kwa milima twakutukuza,
Ewe, Mungu wetu.
Maandishi: Felicia D. Hemans, 1793–1835; yamefanyiwa marekebisho na Edward L. Sloan, 1830–1874
Muziki: Evan Stephens, 1854–1930
Zaburi 95:1–7