Muziki
Mungu Yu Nanyi Wapendwa


40

Mungu Yu Nanyi Wapendwa

Kwa upole

1. Mungu yu nanyi wapendwa,

Kutwa akiwalinda.

Apenda kuwabariki,

Mtapotenda mema.

Abariki, abariki,

Kama mtaamini.

2. Nao malaika juu

Waona kazi zenu,

Na wanaandika yote

Mema, hata maovu.

Penda wema! Penda wema!

Mungu akubariki.

3. Mungu anatufundisha

Kwa sauti ya Roho.

Sikiliza ushawishi,

Uwe furaha yako.

Aminika, aminika

Kwa Mungu na Sayuni.

Maandishi: Charles L. Walker, 1832–1904

Muziki: John Menzies Macfarlane, 1833–1892

Zaburi 37:3–5

Mafundisho na Maagano 41:1

Mafundisho na Maagano 76:5