Muziki
Hamu ya Nafsi ni Sala


77

Hamu ya Nafsi ni Sala

Kwa utulivu

1. Hamu ya nafsi ni sala,

Usemi halisi,

Kama moto, ni hisia,

Yawaka moyoni.

2. Pumzi hushushwa na sala,

Hufuta machozi.

Macho juu hutazama

Kwa Mungu Mwenyezi.

3. Lugha nyepesi ni sala,

Hata kwa mtoto.

Wimbo unaovutia

Mfalme alipo.

4. Sala kweli ni uhai;

Kwa mkristo, hewa.

Mlangoni mwa mauti

Huenda kwa sala.

5. Sauti ya mwenye dhambi,

Akianza toba,

Malaika wafurahi

Kila akiomba.

6. Watakatifu makini

Kupitia sala,

Waupata ushiriki

Wa Baba na Mwana.

7. Tuombapo, si sisi tu;

Na Roho aomba,

Na Yesu kitini juu

Anatuombea.

8. Ewe uliye Ukweli,

Njia na Uzima.

Uyajuaye maombi

Tufunze kuomba.

Maandishi: James Montgomery, 1771–1854

Muziki: George Careless, 1839–1932

3 Nefi 13:5–13

3 Nefi 18:15–20

Yakobo 5:16