Muziki
Ni Upendo Ulioje


108

Ni Upendo Ulioje

Kwa utulivu

1. Ni upendo ulioje

Ulio kwa Baba

Kumtuma Yesu aje

Kuteswa na kufa!

2. Maishaye ya thamani

Kayatoa bure,

Japo hakuwa na dhambi,

Kuokoa wote.

3. Kwa utii akashinda

Zawadi tukufu:

“Kama utakavyo, Baba,”

Alisema Yesu.

4. Yesu alituonesha

Njia ya ukweli,

Kwenye mwanga na uzima

Kwa Mungu mbinguni.

5. Kukumbuka mwili wake

Mkate twakula,

Twaonesha kwa kikombe

Twamwamini Bwana.

6. Ni mkuu na kamili

Wokovu wa Bwana.

Rehema, pendo na haki

Vinaunganishwa.

Ubeti wa 1, 2, 5 na 6 unafaa zaidi kwa ajili ya sakramenti.

Maandishi: Eliza R. Snow, 1804–1887

Muziki: Thomas McIntyre, 1833–1914

Musa 4:1–2

Alma 42:14–15