Muziki
Niongoze


49

Niongoze

Kwa hamasa

1. Yesu, Mkombozi,

Niongoze.

Nakata shauri,

Niongoze.

Hata kwenye giza,

Na kunapokucha.

Uwe wangu mwanga.

Niongoze.

2. Hata kwenye shida,

Niongoze.

Nifundishe wema.

Niongoze.

Nguvu ya wokovu

Iwe kila siku,

Bwana, kinga yangu.

Niongoze.

3. Niwapo na dhambi,

Niongoze.

Nikiwa na jonzi,

Niongoze.

Inapotoweka

Amani na raha,

Nijaze neema,

Niongoze.

4. Kikifika kifo,

Niongoze.

Nitulize moyo.

Niongoze.

Unihurumie

Ili upendowe

Kwako unilete.

Niongoze.

Maandishi na muziki: Orson Pratt Huish, 1851–1932

Alma 38:9

Zaburi 48:14