Muziki
Neno Huleta Amani


10

Neno Huleta Amani

Kwa kuabudu

1. Neno huleta amani

Kwao washirika.

Na mwangaza wa injili

Watuelekeza.

2. Maagizo ni ya Mungu

Anayetujali.

Upendowe mng’aavu

Kwao wafuasi.

3. Uongo humong’onyoka,

Nazo mila ovu.

Wingu lililotishia,

Lakiri u Mungu.

4. Heri tujualo Jina,

Tuziache dhambi.

Roho ataendelea

Kutuweka safi.

5. Punde shetani ashindwa

Na kuisha dhambi,

Shida hazitasumbua,

Wala kutuudhi.

6. Tulivyovipata nusu

Vitakamilika,

Kwani Bwana Mungu wetu

Atavirejesha.

7. Kwa subira twaziponya

Nafsi hadi aje.

Tuzidi kutumikia,

Ukombozi uje.

Maandishi: Mary Ann Morton, 1826–1897

Muziki: Alfred M. Durham, 1872–1957. © 1948 IRI

Zaburi 119:165

Zaburi 119:97–104