Muziki
Tupo Waaminifu wa Imani


147

Tupo Waaminifu wa Imani

Kwa shauku

1. Eti! Vijana wasite

Haki kuitetea?

Huku asumbua mwovu,

Tuache kupambana? La!

[Chorus]

Tupo waaminifu wa imani

Ya wazazi wetu na ya Nabii;

Na kwa Mungu,

Watiifu,

Daima tu waadilifu.

2. Twajua nguvu za giza

Zinampinga Kristo,

Je, watoto wa ahadi

Hawatashika neno? La!

[Chorus]

Tupo waaminifu wa imani

Ya wazazi wetu na ya Nabii;

Na kwa Mungu,

Watiifu,

Daima tu waadilifu.

3. Tutatafuta wokovu;

Ukweli tutashika;

Tutasali tuwe macho

Kwa ari ya ujana. Na’m!

[Chorus]

Tupo waaminifu wa imani

Ya wazazi wetu na ya Nabii;

Na kwa Mungu,

Watiifu,

Daima tu waadilifu.

4. Twapania kustahili

Ufalme wake Kristo,

Na waaminifu wote

Waliotii neno. Na’m!

[Chorus]

Tupo waaminifu wa imani

Ya wazazi wetu na ya Nabii;

Na kwa Mungu,

Watiifu,

Daima tu waadilifu.

Maandishi na muziki: Evan Stephens, 1854–1930

1 Timotheo 4:12

Alma 53:18–21