Muziki
Tumpendao Mungu


18

Tumpendao Mungu

Kwa furaha

1. Tumpendao Mungu,

Njooni kwa furaha.

Tumwimbie nyimbo tamu,

Tumwabudu pamoja.

2. Kuna wale wageni

Wasiojua neno.

Sisi ndio watumishi

Wakutangaza kwao.

3. Mungu ni Mtawala

Wa dunia na mbingu,

Kwa kauli hutuliza

Dhoruba na ghadhabu.

4. Huyu Mwenyezi Bwana,

Ndiye upendo wetu,

Nguvu zake atatuma

Kutupeleka juu.

Maandishi: Isaac Watts, 1674–1748

Muziki: Aaron Williams, 1731–1776

Isaya 12:5

Warumi 8:28