Muziki
Tuko Huru Kuchagua


134

Tuko Huru Kuchagua

Kwa dhati

1. Tuko huru kuchagua

Jinsi tutakavyokuwa;

Mungu hatulazimishi

Kurudi kwake mbinguni.

2. Aita, aelekeza,

Abariki kwa mwangaza,

Ni mkarimu, mzuri,

Na pia halazimishi.

3. Bila uhuru, busara,

Sisi ni kama wanyama,

Ambao hawafahamu

Peponi na jehanamu.

4. Tutumie mamlaka

Kuchagua yale mema;

Anafurahia Kristo

Tukitafuta upendo.

Maandishi: Hajulikani, mnamo 1805, Boston. Yalijumuishwa katika kitabu cha kwanza cha nyimbo za Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu ya Siku za Mwisho, 1835.

Muziki: Roger L. Miller, kuz. 1937. © 1985 IRI

Helamani 14:30–31

2 Nefi 10:23–24