Muziki
Usiku Mtulivu!


117

Usiku Mtulivu!

Kwa utulivu

1. Usiku mtulivu!

Ku kimya, ku ng’avu

Kote kwa mama na Mwana.

Mtukufu, Mwana mwanana,

Lala kwa amani

Lala kwa amani.

2. Usiku mtulivu!

Mchunga ahofu!

Utukufu watokea;

Mbingu yaimba Haleluya!

Azaliwa Kristo!

Azaliwa Kristo!

3. Usiku mtulivu!

Upendo mng’avu

Wang’ara mwako usoni

Na neema ya ukombozi,

Waja Bwana Mungu.

Waja Bwana Mungu.

Maandishi: Joseph Mohr, 1792–1848; Yametafsiriwa na John F. Young, 1820–1885

Muziki: Franz Gruber, 1787–1863

Luka 2:7–14

Alma 7:10–12