Muziki
Katika Siku ya Shangwe


24

Katika Siku ya Shangwe

Kwa furaha

1. Katika siku ya shangwe,

Bwana, twakutukuza;

Hapa ni patakatifu,

Utukufu twaimba.

[Chorus]

Haleluya, Haleluya,

Sauti tuzitoe,

Tuimbeni kwa furaha

Kwa Bwana na Mfalme!

2. Ifungue chemichemi;

Zimwagike baraka,

Kwa wakutumikiao

Kwenye hii dunia.

[Chorus]

Haleluya, Haleluya,

Sauti tuzitoe,

Tuimbeni kwa furaha

Kwa Bwana na Mfalme!

3. Tujenge ufalme wako,

Alisema nabii,

Kwamba wana wa ahadi

Ndipo watapoishi.

[Chorus]

Haleluya, Haleluya,

Sauti tuzitoe,

Tuimbeni kwa furaha

Kwa Bwana na Mfalme!

Maandishi na Muziki: Leroy J. Robertson, 1896–1971. © 1980 IRI

Zaburi 47:6–7

Alma 26:8, 16