Muziki
Tuambizane Mema Daima


132

Tuambizane Mema Daima

Kwa dhati

1. Tuambizane mema daima

Nyumbani au popote;

Kama ndege kati ya maua

Sauti zipokelewe.

Yafariji kwenye majonzi,

Yatutia moyo nguvu,

Na penye wingu la huzuni,

Huleta pendo ng’aavu.

[Chorus]

Kila neno jema litatukumbusha,

Labakia kama kito.

Tuambizane mema daima;

Yawa taswira ya moyo.

2. Kama mwale wa jua Sayuni

Nafsi yanafurahisha;

Kama kisima cha maji safi,

Taratibu yatuwama.

Hivyo kwa sauti karimu,

Urafiki tuujenge,

Mioyo iwe mikunjufu

Na kufurahi popote.

[Chorus]

Kila neno jema litatukumbusha,

Labakia kama kito.

Tuambizane mema daima;

Yawa taswira ya moyo.

Maandishi: Joseph L. Townsend, 1849–1942

Muziki: Ebenezer Beesley, 1840–1906

Waefeso 4:29–32

Mithali 16:24