Muziki
Ukaja Usiku Ule


118

Ukaja Usiku Ule

Kwa uchangamfu

1. Ukaja usiku ule,

Wimbo wa zamani,

Wakiimba malaika

Kwa kupiga vinubi.

“Amani ulimwenguni

Yatoka kwa Bwana.”

Dunia iwe tulivu

Kuwasikiliza.

2. Bado waja na mawingu

Kwa mbawa tulivu,

Na muziki unavuma

Katika ulimwengu.

Nyikani penye huzuni

Wajiinamia,

Juu ya kelele nyingi

Wanawaimbia.

3. Manabii walijua

Siku zitakuja.

Na miaka ipitapo

Yote yatatokea,

Ndipo vitakiri vyote

Bwana wa Amani.

Nayo dunia iimbe

Na wote mbinguni.

Maandishi: Edmund H. Sears, 1810–1876

Muziki: Richard S. Willis, 1819–1900

Luka 2:8–17

Alma 5:50