Muziki
Mungu Mbariki


12

Mungu Mbariki

Kwa sala

1. Mungu mbariki

Mpendwa nabii,

Mpe afya.

Na utuongoze sote

Kwa maneno yake,

Ili tuchague

Yale mema.

2. Na wako ufalme,

Uenee pote

Ufikapo.

Ukweli wawaka,

Nasi twaungana,

Kwa kasi kufika

Kwenye lengo.

3. Tuwe na umoja,

Kama Baba, Mwana,

Kwa amani.

Kwa mioyo yote,

Tusimame sote,

Na milele tuwe

Majasiri.

Maandishi: Bernard Snow, 1822–1894

Muziki: Harry A. Dean, 1892–1987.© 1985 IRI

Mafundisho na Maagano 107:22

3 Nefi 19:23