Muziki
Tubarikie Mfungo


70

Tubarikie Mfungo

Kwa hamasa

1. Bwana tunakusujudu,

Mbele zako twaja,

Tunaomba kwa sauti—

Je, utaongea?

[Chorus]

Tubarikie mfungo

Na nafsi ulishe,

Ili ukawe na sisi

Tufurahi nawe.

2. Tumelisha wahitaji,

Maskini twawapa,

Tukawalaki wageni—

Je, utaongeza?

[Chorus]

Tubarikie mfungo

Na nafsi ulishe,

Ili ukawe na sisi

Tufurahi nawe.

3. Kama mashahidi twaja

Kukupa shukrani,

Kwa kutenda miujiza,

Bwana tubariki.

[Chorus]

Tubarikie mfungo

Na nafsi ulishe,

Ili ukawe na sisi

Tufurahi nawe.

Maandishi: John Sears Tanner, kuz. 1950. © 1985 IRI

Muziki: James B. Welch, kuz. 1950. © 1985 IRI

Isaya 58:6–11

Mafundisho na Maagano 59:12–21