Muziki
Nabii Mpendwa


14

Nabii Mpendwa

Kwa hamasa

1. Nabii mpendwa, twamuomba

Akupe faraja, Mungu Baba.

Miaka ijavyo na uzee,

Na mwangaza wako uangaze,

Na mwangaza wako uangaze.

2. Tunakuombea mioyoni,

Ukapewe nguvu na Mwokozi

Ya kutuongoza kila siku,

Ya kuiangaza njia yetu,

Ya kuiangaza njia yetu.

3. Tunakuombea, twakupenda,

Na maombi yetu yasikika.

Ubarikiwe na Mungu wetu,

Na akupatie kila kitu,

Na akupatie kila kitu.

Maandishi: Evan Stephens, 1854–1930

Muziki: H. A. Tuckett, 1852–1918; umefanyiwa marekebisho na Evan Stephens, 1854–1930

Mafundisho na Maagano 107:22