146
Tumaini la Sayuni
Kwa shauku
1. Tumaini la Sayuni,
Kizazi cha ahadi,
Ona, Bwana aamuru,
Pambaneni vitani!
[Chorus]
Israeli, simama,
Onya, “Chunga na omba!”
Angamiza adui
Na upanga wa haki.
2. Ona wingi wa adui,
Kwenye safu za dhambi.
Israeli tupambane;
Tusikose ushindi!
[Chorus]
Israeli, simama,
Onya, “Chunga na omba!”
Angamiza adui
Na upanga wa haki.
3. Sayuni, pinga maovu
Kwa haki na upanga!
Tuzizime mbinu zote,
Twendelee kushinda.
[Chorus]
Israeli, simama,
Onya, “Chunga na omba!”
Angamiza adui
Na upanga wa haki.
4. Punde vita vitaisha;
Adui, chini yenu.
Songa wana wa Sayuni;
Taji, yenu thawabu.
[Chorus]
Israeli, simama,
Onya, “Chunga na omba!”
Angamiza adui
Na upanga wa haki.
Maandishi: Joseph L. Townsend, 1849–1942
Muziki: William Clayson, 1840–1887
Waefeso 6:10–18