Muziki
Tumaini la Sayuni


146

Tumaini la Sayuni

Kwa shauku

1. Tumaini la Sayuni,

Kizazi cha ahadi,

Ona, Bwana aamuru,

Pambaneni vitani!

[Chorus]

Israeli, simama,

Onya, “Chunga na omba!”

Angamiza adui

Na upanga wa haki.

2. Ona wingi wa adui,

Kwenye safu za dhambi.

Israeli tupambane;

Tusikose ushindi!

[Chorus]

Israeli, simama,

Onya, “Chunga na omba!”

Angamiza adui

Na upanga wa haki.

3. Sayuni, pinga maovu

Kwa haki na upanga!

Tuzizime mbinu zote,

Twendelee kushinda.

[Chorus]

Israeli, simama,

Onya, “Chunga na omba!”

Angamiza adui

Na upanga wa haki.

4. Punde vita vitaisha;

Adui, chini yenu.

Songa wana wa Sayuni;

Taji, yenu thawabu.

[Chorus]

Israeli, simama,

Onya, “Chunga na omba!”

Angamiza adui

Na upanga wa haki.

Maandishi: Joseph L. Townsend, 1849–1942

Muziki: William Clayson, 1840–1887

Waefeso 6:10–18

2 Nefi 28:7–8, 20–28