Muziki
O! Kisima Cha Baraka


174

O! Kisima Cha Baraka

Kwa kuomba

1. O! Kisima cha baraka,

Imbisha moyo wangu;

Tiririko za rehema,

Zaniita kusifu.

[Chorus]

Nifundishe tenzi nzuri,

Ziimbwazo uliko;

Mlima – wangu msingi —

Nasifu pendo lako.

2. Naita Ebenezeri,

Hapa nimefikia,

Nako kwa yako mapenzi,

Nyumbani nitafika.

[Chorus]

Kupotea ni mwepesi,

Hata kumwacha Mungu;

Moyo wangu, Ee Mwokozi,

Ufunge kwako juu.

3. Alinitafuta Yesu

Nikiwa ugenini;

Akamwaga yake damu

Kunitoa jangani.

[Chorus]

Kupotea ni mwepesi,

Hata kumwacha Mungu;

Moyo wangu, Ee Mwokozi,

Ufunge kwako juu.

4. O! Yanilazimu kuwa

Daima mwiwa wako!

Ufungavyo wako wema,

Nifunge wangu moyo.

[Chorus]

Kupotea ni mwepesi,

Hata kumwacha Mungu;

Moyo wangu, Ee Mwokozi,

Ufunge kwako juu.

Maandishi: Robert Robinson, 1735–1790

Muziki: John Wyeth, 1770–1858