Muziki
Wapendwa wa Mchungaji


126

Wapendwa wa Mchungaji

Kwa utulivu

1. Wapendwa wa Mchungaji,

Ni kondoo wapendwa;

Tunu pendo awapalo,

Tunu kuliko fedha.

Wapendwa wa Mchungaji,

Na kondoo “wengine”;

Milimani awasaka,

Hata kina chochote.

[Chorus]

Jangwani watangatanga,

Wasumbuka wapweke;

Aenda kuwakomboa,

Zizini warudishwe.

2. Wapendwa wa Mchungaji,

Ndio wanakondoo;

Kuna wanaopotea,

Wadhoofika huko.

Ona, Mchungaji Mwema,

Asaka wapotevu,

Awarudisha kwa shangwe,

Na kwa gharama kuu.

[Chorus]

Jangwani watangatanga,

Wasumbuka wapweke;

Aenda kuwakomboa,

Zizini warudishwe.

3. Wapendwa wa Mchungaji,

Ni “tisini na tisa.”

Apenda wapoteao,

Tumaini wakosa.

Sikia! Wito wa moyo,

Kwa upole asihi:

“Hutafuti mpotevu,

Aliye mbali nami.”

[Chorus]

Jangwani watangatanga,

Wasumbuka wapweke;

Aenda kuwakomboa,

Zizini warudishwe.

4. Malisho yanavutia;

Maji yenye uhai.

Bwana, kwa ari twajibu,

“Ndiyo, tunakubali!

Tufanye wachunga wako;

Tupe pendo la kina.

Tutume mbali jangwani,

Kondoo kuwasaka.”

[Chorus]

Jangwani watangatanga,

Wasumbuka wapweke;

Twendeni kuwakomboa,

Zizini warudishwe.

Maandishi: Mary B. Wingate, 1845–1933

Muziki: William J. Kirkpatrick, 1838–1921

Luka 15:4–7

1 Petro 5:2–4