116
Malaika wa Juu
Kwa furaha
1. Malaika wa juu
Makondeni waimba,
Na milima yajibu
Miwangwi ya furaha.
[Chorus]
Utukufu kwake Mungu juu.
Utukufu kwake Mungu juu.
2. Wachungaji, kunani?
Mbona nyimbo mwaimba?
Ni taarifa gani
Zinazowavutia?
[Chorus]
Utukufu kwake Mungu juu.
Utukufu kwake Mungu juu.
3. Njooni mumuone
Yule anayeimbwa;
Njoo, msujudie
Mtoto, Kristo Bwana.
[Chorus]
Utukufu kwake Mungu juu.
Utukufu kwake Mungu juu.
Maandishi: Wimbo wa Krismasi wa Ufaransa, mnamo 1862
Muziki: Wimbo wa Krismasi wa Ufaransa
Luka 2:8–20
Zaburi 95:6