Muziki
Sayuni Nzuri Mbinguni


23

Sayuni Nzuri Mbinguni

Kwa upole

1. Sayuni nzuri mbinguni;

Napenda mji mzuri;

Mizuri milango yake;

Hekalu – Mungu nuruye;

Aliyenipatanisha,

Milango aifungua.

[Chorus]

A! Sayuni, ni kuzuri;

Mji Sayuni;

Sayuni, kwake Mungu!

2. Kuzuri mbinguni kote;

Hata malaika wote;

Nzuri nazo tumbuizo;

Nzuri tarumbeta zao;

Nitaimba na umati,

Miguuni pa Mwokozi.

[Chorus]

A! Sayuni, ni kuzuri;

Mji Sayuni;

Sayuni, kwake Mungu!

3. Mazuri mataji yao,

Matawi watandazayo;

Wazuri wakombolewa,

Wote wanaoingia;

Nitaingia kwa hamu

Kwenye pumziko langu.

[Chorus]

A! Sayuni, ni kuzuri;

Mji Sayuni;

Sayuni, kwake Mungu!

Maandishi: George Gill, 1820–1880

Muziki: Joseph G. Fones, 1828–1906

Ufunuo 7:9–17

Ufunuo 21:2, 21–23