Muziki
Twamjia Bwana Kuomba Baraka


43

Twamjia Bwana Kuomba Baraka

Kwa furaha

1. Twamjia Bwana kuomba baraka;

Hukanya, hutupa mapenzi yake;

Sasa wasumbufu wakoma maovu.

Bwana tumsifu;

Yu na waja wake.

2. Yu nasi kutuongoza, Mungu wetu,

Falme kuitunza na kustawisha;

Siku hadi siku vita tumemudu;

Bwana, upo nasi;

Tukuzwa daima!

3. Tunakusifu, kiongozi mshindi,

Na tunaomba utuhami tena.

Tuepushe sote na adui yule.

Usifiwe juu!

Tuhurishe Bwana!

Maandishi: Hajulikani, Uholanzi, mnamo 1626; yametafsiriwa na Theodore Baker, 1851–1934

Muziki: Hajulikani, Uholanzi, mnamo 1625; umepangiliwa na Edward Kremser, 1838–1914

Zaburi 100:4–5

Isaya 12:1–6