Muziki
Sasa Kwa Ustahifu


100

Sasa Kwa Ustahifu

Kwa unyenyekevu

1. Sasa kwa ustahifu,

Kwa upole sujudu.

Tathminia, wazia

Niliyokufanyia.

Kwa damu yangu nyingi,

Na maumivu mengi,

Kwa mwili wangu pia

Nimekushuhudia.

2. Mkate huu kwenu,

Ni kama mwili wangu;

Maji au divai,

Damu msalabani.

Nilichofanya, ewe

Mwanadamu usife,

Pale Fuvu la Kichwa,

Ni kifo kupitia.

3. Shauri moyo wako,

Tulia na nduguzo.

Wasamehe wengine

Hata nikusamehe.

Kwa sala ya imani

Shida zako kabidhi,

Na neema ya Roho

Iwe kisima kwako.

4. Kwenye Kiti cha Enzi,

Kwenu ni mtetezi;

Upendo wangu kwako,

Hata hauna mwisho.

Kuwa na utiifu,

Daima mwangalifu,

Kwangu uwe mwamini,

Kwako niwe Mwokozi.

Maandishi: Joseph L. Townsend, 1849–1942

Muziki: Ebenezer Beesley, 1840–1906

Mafundisho na Maagano 45:3–5

Mafundisho na Maagano 19:16–19