Muziki
Twarudisha Kwako


127

Twarudisha Kwako

Kwa shukurani

1. Twarudisha kwako

Baraka adhimu;

Twajua tulivyo navyo

Umetupa, Mungu.

2. Wingi wa neema,

Kama wakadamu,

Twapokea na kuleta

Milimbuko yetu.

3. Kuwapa faraja,

Kupoza taabu,

Wanyonge kuhudumia

Ndiyo kazi kuu.

4. Twaamini neno,

Japo tu dhaifu;

Kila tuwatendealo,

Twatenda kwa Yesu.

Maandishi: William Walsham How, 1823–1897

Muziki: Hajulikani, mpangilio na Lowell Mason, 1792–1872, na George J. Webb, 1803–1887

Mithali 3:9

Mathayo 25:34–40